Wizara Ya Maji

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Singida

SUWASA IMEPOKEA WAKAGUZI KUTOKA OFISI YA RAIS TUME YA UTUMISHI WA UMMA


Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Singida (SUWASA) imepokea Wakaguzi kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma ambao wamefika katika ofisi za SUWASA kwa ajili ya ukaguzi wa kiutendaji katika maeneo mbalimbali ya kiutumishi.

Wakaguzi hao ambao wameongozwa na Mkaguzi Kiongozi Bi. Sheila Dachi wameeleza kuwa, huu ni Ukaguzi wa kawaida wa Mwaka 2024/2025 ambapo lengo ni kuhakikisha sheria za kiutumishi zinazingatiwa katika utendaji.